"SITOI NG'O FEDHA ZA RAMBIRAMBI ZA ASKOFU KULOLA KWASABABU NIMEDHALILISHWA".MZEE WA UPAKO.
Mchungaji
wa Kanisa la GRC, Anthony Lusekelo ‘ Mzee wa Upako’ amesema hatatoa
ng’o fedha za rambirambi za Askofu Moses Kulola kutokana na
kudhalilishwa kulikofanywa na wahusika wa kukusanya fedha hizo.
Mzee
wa Upako alisema badala yake fedha hizo shilingi milioni 15 sasa
zitatumika kutibu maumivu aliyoyapata kutokana na vyombo vya habari
kuandika utata juu ya ahadi yake ya kutoa rambirambi hizo.
“Kwanza
mimi mtu aliyetajwa kuwa angekusanya fedha hizo ambaye ni Mweka Hazina
wa Kanisa la EAGT, Mchungaji Praygod Mgonja simjui kwa sura,
nilishamueleza njia gani muafaka ya uwasilishaji wa fedha hizo, badala
yake akatumia vyombo vya habari kunidhalilisha.
“Nilimwambia
Mchungaji Mgonja kuwa shilingi milioni kumi na tano siyo kama shilingi
laki tatu; Zinapaswa kuwa na utaratibu unaoeleweka wa kutolewa.
Nikamwambia mama Kulola (mke wa marehemu) azifuate mwenyewe ili aniombee
baraka, akasema sawa, sasa nashangaa ananidhalilisha,” alisema Mzee wa
Upako.
Alisisitiza
kauli yake hiyo pia kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno wa simu kwa
mwandishi wa habari hii kuwa hatatoa ng’o fungu lake aliloliahidi.
Aliongeza
kuwa kwa sasa ameghairi kutoa fedha hizo kwa kuwa anadhani kuna njama
fulani ambazo hakuzitaja na kwamba fedha hizo sasa atazitumia kutibu
majeraha aliyoyapata baada ya habari kutoka katika vyombo vya habari.
Mchungaji
Mgonja alisema kuwa hajapokea rambirambi za Mzee wa Upako ambazo ni
shilingi milioni 15 na wengine walioahidi akiwemo Mchungaji Josephat
Gwajima aliyeahidi kutoa shilingi milioni 10 na Mchungaji Getrude
Lwakatare (shilingi milioni moja) walishatoa.
No comments:
Post a Comment