Marekani: Al-Liby alikamatwa kihalali

https://fbcdn-sphotos-h-a.akamaihd.net/hphotos-ak-prn2/1375680_662915860393749_2138091497_n.jpg


Marekani imesema kuwa gaidi aliyekamatwa na vikosi maalum vya Marekani nchini Libya anzuiliwa katika meli ya kijeshi katika bahari ya Mediterranea.

Abu Anas al Libi, anadaiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la al-Qaeda na amekuwa akisakwa kwa kuhusika na mashambulizi ya kigaidi dhidi ya balozi za Mareakni nchini Kenya na Tanzania mwaka 1998.

Waziriu wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry alisema kuwa hakuna makosa kwa kumkamata Al Libi kwani alikuwa anasakwa kihalali kwa vitendo vya kigaidi

Awali viongozi wakuu wa Libya walitaka maelezo kutoka kwa Marekani, baada ya Abu Anas al Libi anayedaiwa kuwa mfuasi wa al-Qaeda kutekwa mjini Tripoli na makamando wa Marekani.

Mwanamme huyo, alikuwa anasakwa kwa kuhusika na mashambulio dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania miaka 15 iliyopita.

Wizara ya Ulinzi ya Marekani inasema Anas al Libi sasa anazuwiliwa nje ya Libya.

Kakake amesema kukamatwa kwake kulikuwa kitendo cha uharamia.

Jumamosi makamando wa Marekani piya walishambulia nyumba mjini Barawe, Somalia, ambayo inadaiwa kutumiwa na kiongozi mmoja wa kundi la al-Shabaab aliyehusika na shambulio katika jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi, lakini walishindwa kumpata.

Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Marekani, John Kerry, amesema kuwa mashambulio hayo mawili yanaonesha dhamira ya serikali ya Marekani kuwasaka wale wanaohusika na ugaidi.

No comments: