MTOTO ACHOMWA MOTO NA MAMA YAKE KWA TUHUMA ZA KUIBA MAYAI YA KUKU HUKO JIJINI MBEYA....!!
WIMBI la ukatili dhidi ya watoto linazidi kushika kasi jijini hapa baada
ya mtoto, Emilly George (7) Mkazi wa kijiji cha Ruanda wilaya ya Mbeya
kuunguzwa vibaya mikono na mama yake mzazi, Elisia Mwasile (41) kwa maji
ya moto kisha kufungiwa ndani kwa siku saba.
Akizungumza huku akiwa
anatetemeka kwa hofu, mama wa mtoto huyo, Elisia alisema kuwa chanzo cha
kumchoma mtoto wake ni kutokana na kuchoshwa na malalamiko ya majirani
zake waliokuwa wakimtuhumu mtoto huyo kujihusisha na vitendo vya wizi
vya kuiba fedha na mayai ya kuku.
Mama mzazi wa mtoto aliyechomwa moto ELESIA MWASILE[41] akipelekwa kituoni na wanausalama
Tukio la mwisho lililosababisha
mtoto huyo kuchomwa na maji ya moto ni la hivi karibuni ambapo majirani
walimwambia mama huyo kwamba mtoto wake ameiba mayai kutoka kwa majirani
zake.
Baada ya kuunguzwa kikatili, mtoto huyo alifungiwa ndani kwa
siku saba bila matibabu yoyote hali iliyowafanya majirani kuanza
kumtafuta wasijue alipo.
Baada ya kutomuona mitaani, majirani hao walitoa taarifa ofisi ya kijiji ili kubaini alipo mtoto huyo.
Uongozi
wa kijiji baada ya kupata taarifa hizo ulifanya upekuzi na kumkuta
mtoto huyo akiwa amefungiwa ndani huku akiwa na majeraha makubwa katika
mikono yake ndipo taarifa ilitolewa Kituo cha Polisi Mbalizi na mama
huyo kukamatwa.
Baada ya kukamatwa mama huyo alikabidhiwa kwa Dawati
la Polisi Jinsia na Watoto chini ya Kiongozi wa Wilaya, Pudensiana Baitu
na mwenyekiti wake, Mary Gumbo ambaye muda mwingi alikuwa akiangua
kilio kutokana na kitendo alichofanyiwa mtoto huyo.
Hadi tunakwenda
mitamboni mama mzazi wa mtoto huyo alikuwa akihojiwa na Polisi Kituo
Kikuu cha jijini Mbeya na anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma
hizo.
Mtoto Emilly amelazwa katika Hospitali ya Rufaa wodi namba tano akiendelea kupatiwa matibabu.
Vitendo
vya unyanyasaji vimeendelea kukemewa jijini Mbeya na asasi mbalimbali
kutokana na watoto kubakwa, kulawitiwa, kufanyishwa kazi za ndani na
baadhi yao kupata ulemavu wa kudumu ikiwemo kupoteza viungo.
No comments:
Post a Comment