PETE YA NDOA IMENIPONZA....NDOA IPO HATARINI.


Wadau nipo njia panda naombeni ushauri wenu, nimefanya kosa kubwa na nalijutia Tafadhali naomba ushauri badala ya kunituhumu.

nilikuta na demu mmoja tulisoma naye chuo kitambo alikuwa demu wangu for time being, so baada ya miaka kadhaa tukaja kukuta sehemu, shetani akanipitia nikavunja amri ya sita naye.

Baada ya kurudi home nikagundua sina pete, nikajaribu kukumbuka nilipoiweka sikupata majibu.

Baada ya siku kadhaa yule demu akzidi kunisumbua na kutaka niwe karibu naye sana lakini nikaona si vyema maana anaweza kusababisha mtafaruku kwa ndoa yangu

Baada ya kuona nampotezea akaniambia sasa unajifanya mjanja pete yako ni nayo na nahitaji sh 500,000 cash ama sivyo naharibu kwa mkeo kwamba pete ninayo na ulinikopa.

Kibaya zaidi wife aliniuliza pete umepeleka wapi nikadanganya nimeisahau ofisini nilikuwa nafungua printer sasa pete ikawa inani disturb nikaivua , nilipoenda jumatatu nikamwambia nahisi wahudumu wa usafi wameiiba maana siiona pale nimeiweka naendelea na uchunguzi.

Mwanzo nilimpuuzia lakini mshenzi yule kapeleleza hadi wife anapofanya kazi na kapata simu yake, juzi kampigia kamwambia "naomba mkumbushie mumeo deni langu mimi xxxxx nampigia simpati" halafu akakata simu.

Niliporudi wife kanibana nikamwambia ni mambo ya kazi tu akataka kujua no yake kaipataje, nikazuga zuga na ubabe wa kiume yakaisha

Nikipiga akili nimuendee Polisi naona kama kitanuka na wife atajua

Nikifikiria kumlipa akili hainipi kabisa....kilo tano?

Sijui nimueleze wife ukweli?

Nimejaribu kumpigia simu na kumbembeleza kagoma anachohitaji ni kilo tano au aniharibie kwa wife.

Tafadhali ushauri wakuu lawama na madongo hayatanisaidia.

No comments: